Hatimaye Timu ya Serengeti Boys imefuzu michuano ya Afrika...!!

October 02, 2016 0 Comments



Timu ya vijana wa Tanzania chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Boys) leo wamejihakikishia safari ya kushiriki michuano ya Afrika baadaya ya kutoka sare kwenye mechi ya marudiano dhidi ya Timu ya vijana Congo Brazzavile. Awali mechi ya awali ambayo Timu ya Vijana ya Tanzania Serengeti Boys wakiwa nyumbani, walishinda 3 -2 dhidi ya timu hiyo ya Congo na hivyo kwa ushindi wa leo Vijana hao wamefuzu michuano hiyo.

Kabla ya kuwaondoa vijana wa Congo Brazzavile, vijana hao wa Serengeti Boys waliwaondoa timu ya Afrika Kusini.

0 comments: